HUKUMU YA HAKI SEHEMU YA 5
HUKUMU YA HAKI
SEHEMU YA..5
Mtunzi Ayubu Henry
ILIPOISHIA....
umesema kuwa ni Penina Mwasera?". jaji aliuliza.
"ndiyo, kwani unamfahamu?"
eddi aliuliza.
"Ndiyo namjua tena namjua".
Edisoni alisema akiwa anatetemeka na machozi yakimtoka.
"namjua....namjua.... namjua
Penina Mwasera namjua kabisa namjua kabisa namjua"
jaji aliendelea kusema kwa pupa huku machozi yakichuruzika na akiwa anaria
kitendo ambacho kilimusisimua kila mmoja pale nakushangaa na kupata shauku la kujua nini kinaendelea na kumjua huyo Penina Mwasera
ENDELEA......
"baba kwani huyo penina ni nani" jesika aliuliza.
"mwanangu unataka kumfahamu huyu Penina" Eddi aliuliza.
"Hapo nyuma kidogo kama miaka 28 iliyo pita kuna mambo mengi yaliyo tokea kijijini kwetu wasichana baada ya kukosa shule wengine walianza kwenda kigoma mjini na wengine mikoa mingine kwenda kutafta pesa za kuwa tunza, wakati huo walitoka wasichana wengi sana,
siku moja nikiwa na dada yangu tulikuwa tumekaa sehemu tunajaribu kupangilia tufanyeje kwa sababu wakati huo tulikuwa hatuna wazazi tulikuwa yatima,
wazazi wetu walifariki mwaka mmoja ulio kuwa umepita kwa wakati ule.
Mama yetu aliitwa Jesika Andrew na baba yetu aliitwa Mwasera,
jina mwasera lilitokana na wazazi wake walio muza yaani babu na bibi zetu
babu aliitwa Mwamuzi Isaya na bibi aliitwa Selina Rashidi
walichukua majina yao la baba na la mama wakajumlisha vyanzo vya majina yao baba walichukua Mwa na mama wakachukua Se na mwisho wakaongeza Ra wakapata Mwasera.
ila nasikitika kuwa nasikia habari zao wala sikuwahi kuwaona nao nasikia walisha kufa.
siku hiyo tulivu tulikuwa tunajaribu kufikiria tufanye nini tukashauriana kuwa tusambae mimi niende kwa mkuu wa mkoa kuomba musaada kweri mimi nilienda kuomba musaada kwakuwa mkuu yule bwana Aridi Yusufu mkuu wa mkoa miaka ile
hakubahatika kuzaa alinichulia kama mtoto akaamua kunisomesha.
muda mchache ulipita dada yangu alinitumia barua nayo hii hapa huwa kila napoenda naendanayo barua hii imeandikwa.
Kwako kaka mpendwa Edisoni, najua kuwa hautapenda kukaa mbari na mimi lakini itakulazimu ukae mbari nami,
mimi nimekaa nakuwaza nimeamua kwenda mjini kutafta maisha na kuna mtu kaja kunichukua anasema ananipeleka kufanya kazi hotelini, nafikiri nikienda kule naweza kupata pesa na baadae nikaendelea kiuchumi.
naenda Arusha japo kuwa bosi simujui ila naenda kule kwa kupelekwa na mtu kutoka hukohuko Arusha nadhani ni mtu alie tumwa kuja kutafta watu wakuweza kuwasaidia.
namaliza kwa kusema nakupenda sana.
wako mpendwa Penina Mwasera."
jaji aliwasomea huku akihisi kupasuka kwa sababu ya musongo wa mawazo na kutetemeka.
baada ya kuwasomea akaendelea
"baada ya mda mwingi kupita niliona vema kuweza kwenda Arusha kumtafta dada yangu rakini sikumpata nilijitahidi kutafta kila hoteli lakini sikumpata.
Baada ya muda tulihamia Dar tukaishi huku nikaamini kuwa dada alisha kufa na itakuwa ngumu hata wa kujua alifia wapi.
miaka mingi imepita kumbe wewe ni mpwa wangu??
mtoto wa dada yangu??
Essi njo mwanangu unikumbatie mimi na wewe ni familia moja wewe ni familia yangu".
walikumbatiana wote wakiwa wanalia
kila mmoja hakuamini kumbe Esilomu ni mtoto wa Penina dada yake Edisoni hakuna alie kuwa analijua hilo,
walikumbatiana wote wawili yaani Esilomu na Edisoni kila mumoja analia akisema "siamini ....siamini."
Dakika tano zilikatika wakati wakiwa wote wanakumbatiana kumbaiana kwa uvhungu.
jaji alisema
"Essi usijali wewe ni familia yangu siwezi kukuacha upotee kama alivyo potea mdogo wangu Penina nikiwa naona, niko tayari kukusaidia usijari mwanangu, wewe ni sawa na mwanangu" jaji alisema huku machozi yakimutoka.
baada ya kusema yote hayo akasema "Essi bado siku mbili ili wewe unyongwe lakini niko tayari kukusaidia na tena niko tayari kukupeleka sehemu yeyote ili uwe huru.
ila nakuomba uniache nikajaribu kutafta mbinu ya kukusaidia, sababu ukweri nimesha upata wewe usijari,
kesho utatoka humu jera by any means".
alimaliza akiwa anaamka na kuanza kutembea huku nyuma akimfata Jesika, mda wa dakika mbili na sekonde kadha walifika kwa bwana jera.
"ndugu yangu ninajambo la kuongea ila ni kwaajiri yangu tuu na wewe, je tunaweza kutoka kidogo?" Jaji aliuliza
"ndiyo usijari wewe ni kama ndugu nikikumbuka ulivyo nisaidia mambo mengi kwa nini nisikusilikilize?" bwana jera alisema.
"jesika naomba ubaki hapa tunakuja dakika sii nyingi sawa baby?" baba alisema.
"ok dady" Jesika alisema huku Edisoni na bwana Jera wakielekea nje kwa mazungumzo.
Wote walikuwa kimya kama dakika mbili ndipo bwana jera akauliza "Ndiyo" aliashilia kutaka kujua zaidi kinacho msibu Edisoni.
nae eddi hakusita akasema "ndugu yangu kuna jambo ambalo naweza kusema ni kubwa kuzidi mamlaka yangu na pia kuzidi kabisa ufikiliaji wangu" Eddi alinyamanza na kuendelea
"nakosa hata nianzie wapi ndugu yangu kukuelezea, sababu ni jambo zito sana".
bwana jera akasema baada ya edisoni kuwa na kigugumizi kikubwa kulingana na tatizo lake."jaji wewe nikama ndugu yangu tumesaidizana mengi maishani sidhani kama matatizo yako kuwa hayani husu, yananihusu kabisa wewe niambie....." hakumalizia Edisoni akadakia nakusema.
"ndugu yangu kama unavyo jua sina baba wala mama ninaishi hivihivi nilivyo,
miaka takilibani ishirini na nane nilikuwa naishi na dada yangu, aliitwa penina nilimpenda sana!! sikupenda akae mbali nami, najua lilikua jukumu langu la kumulinda dada yangu ila sikufanikiwa mara tu baada ya kuchukuliwa na mtu wa kunilea na kutaka kunisomesha dada yangu alinitumia barua, najua barua ile hakuandika yeye aliandikiwa kilicho nifanya niumie zaidi ni pale milipo kumbuka dada yangu hajui kusoma lakini kanitumia barua, siwezi nikaitupa nitatembea nayo mpaka kifo changu" jaji alinyamanza kidogo huku akijifuta machozi ambayo yalikuwa yameanza kuchirizika akaendelea na simulizi ambayo imeanza kumuingia bwana jera.
"barua hiyo ilinijulisha kwamba yeye dada yangu amepata mtu wa kumpeleka Arusha kwa shughuri moja ya Hotelini, yaani kama kufagia na mambo madogo madogo yaani zile kazi ambazo mtu ambae haja soma anaweza kufanya. sikuweza kumzuia kwa sababu sikumuona hiyo ilikuwa mara yangu ya mwisho kumusikia tena wala kumuona.
miaka kadha nilienda Arusha wakati hatujahamia huku dar es salaamu. Nilifika kule Arusha kumtafta dada yangu lakini sikumpata takilibani kila Hoteli kubwa niliingia lakini sikumpata, hivyo nilikaa nikiwa najua kuwa dada yangu sito muona tena, ila reo sijui kwa nini hili limetokea mtu alie shikiliwa na polisi kwa mauaji na mwisho akakosa hata ndugu wa kumsimamia katika kesi yake kumbe ni mtoto wa dada yangu.
dada yangu kabisa ndiye mama yake Esilomu Ngware mtuhumiwa kwa makosa ya uuaji wa watu wawili vigogo." jaji alisema huku akiashiria kuna mengi yanamuhusu Esilomu.
bwana jera hakuamini alihisi anaota kwa yale aliyo ambiwa "kumbe Esilomu ni ndugu yake Edisoni? hii ni ajabu sana, kwakweri mungu ni waajabu sana yaani watu walio poteana wanakuja kujuana kwenye shida mungu wewe ni waajabu"bwana jera alijiwaza huku akimuangalia jaji aliekuwa anajifuta machozi ya furaha na maswari mengi.
mda mchache kupita bwana jera akauliza "sasa ndugu yangu kwanza pole na matatizo yaliyo kusibu ila napenda kukupa pole ila pia asante kubwa ni kwa Mungu alie juu maana yeye ndiye alie panga hili litokee na kama alivyo panga basi ni suara la kujua pia atamaliza yeye mwenye mungu.
ila pia nasikitika kukwambia kwamba kesho Esilomu Ngware atahamishwa kupelekwa jera nyingine ambapo hupelekwa watu maarumu kama wanao nyongwa au wenye kifungo chamaisha." Jaji alistuka sana baada ya kuambiwa kesho inatakiwa ahamishwe Esilomu kupelekwa sehemu nyingine.
"kwani atapelekwa wapi?" eddi aliuliza
"huturusiwi kupasema wala kusema siri hii ila ninaweza kukuambia usijari ila kwa maelewano kwamba hutasema." bwana jera alisema baada ya kusema jaji akadakia "najua lazima mfanye siri lakini naomba nikuulize kitu kimoja inamaana huko atapelekwa saa ngapi?"
"hawana muda maalumu ila mala chache huwa wanawapeleka saa nne za asubuhi ila mala nyingi huwapeleka saa kumi na mbili arufajili , kwa hiyo siwezi kujua moja kwa moja atapelekwa saa ngapi.
lakini Eddi naomba niurize"
"uliza tuu" jaji alijibu.
"kwa maelezo yake nikweri kwamba aliua?" bwana jera aliuliza.
"ndiyo aliua , hakika yeye ni muuaji ila ana sababu!!!" jaji alijibu.
"zipi hizo sababu?" bwana jera aliuliza
"ndugu yangu natamani kukuambia lakini nihistoria ndefu huu siyo muda wake nitakuambia ngoja nifanye kwanza mchakato wa kumsaidia kwanza kijana huyu". alisema huku wakiwa wanarundi ndani ambapo walimuacha Jesika,
walikuta jesika anabadilishana mawili matatu na walinzi walio kuwepo pale.
"sasa unaenda wapi kwa sasa?" bwana jera aliuliza.
"naenda kwa majaji wenzangu kuwaeleza habari hizi kwa sababu mimi nahitaji kunyongwa kwake kusitishwe harafu nitatafta namna ya kufanya upelelezi kisha niuweke wazi ushenzi na uchafu ulio kuwa unafanywa na hawa vigogo wawili ambao walionekana watu muhimu kumbe ni simba mwenye ngozi ya kondoo."
maneno yale yalimfanya bwana jera aamini kitu moyoni mwake kwamba yawezekana kunasababu ya yeye kufahu na kuwajua kiundani hawa vigogo wawili walio kufa.
Baada ya mazungumuzo machache baina ya jaji na bwana jera waliagana na jaji kutaka kuondoka bwana jera akasema " nakutakia majukumu mema yenye mafanikio"
"nashukuru ndugu yangu nadhani tutaonana wakati mwingine" jaji alisema wakaanza safari.
wakiwa safarini Edisoni hakuongea kitu ila baada ya dakika chache Jesika binti mwenye uzuri wa kipekee, binti mwenye shingo la twiga sauti nyororo akasema "baba kwani tunaelekea wapi kwa sasa?"
"mwanangu tunaelekea ikuru kwa raisi" jaji alibu
"ikuru baba?"
"ndiyo tunaenda ikuru" Eddi ali sisitiza swala hili
Jesika alimuangalia babayake alie kuwa ameshika usukani vyema.. binti huyu aligundua kuwa hakika baba yake alikuwa akimaanisha kile alicho kuwa akikiongea.
"Nilazima Esilomu nimsaidie kwa tatizo hili aliro naro, kwanza ni ndugu yangu ni mtoto wa dada yangu ila harafu niwajibu wangu kusimamia sheria lazima haki itendeke siwezi kumuacha kabisa afe nikiwa naona ni mtu wa muhimu kwangu, nadhani nikifanya mchakato kesho asihamishwe na kesho kutwa asinyongwe basi nitakuwa nimefanya vizuri itanibidi nifanye uchunguzi kuhusu maisha ya hawa watu wawili ndipo nitakapo kuwa nimempa uhuru Esilomu kinyume na hapo atanyongwa tuu, siwezi kuruhusu hili dada yangu alikwenda ila mwanae hawezi kwenda kingali nipo hai..". jaji alikuwa akijiwaza huku akiwa anaendesha gari kwasi kuelekea ikuru kwa raisi wa jamhuri ya muuangano wa tanzania.
ITAENDELEA........
MPENZI MUSOMAJI ENDELEA KUFUATILIA KISA HIKI CHA KUSISIMUA.
LIKE NA COMMENT.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO SWARI JE EDISON ATAWEZA KUMSAIDIA ESILOMU