HUKUMU YA HAKI SEHEMU YA 4
HUKUMU YA HAKI
SEHEMU YA..4
Mtunzi Ayubu Henry
ilipo ishia .
. mimi nilimuuliza maisha yake yako nilidhani nimafupi kumbe marefu sana na pale alipo hana wazazi na hamjui baba yake nawala hata mama yake mwenyewe hakuwahi kumwambia mwanae kuwa baba yake ninani maana alikufa kingali Essi ana umri wa mwaka mmoja ilikuwa mwaka 1989 ndipo mama yake alipo faliki kuhusu jina la mama yake hajaniambia lakini alisematena kwamba mama yake alikuwa ni kahaba alipo kufa alichukuliwa na mzee mmoja anajulikana kwa jina la Ngwale alimulea ila pia yule mzee alikufa kwa mazingira ya kutatanisha na historia yake huyo mzee nikwamba alikuwa ni shoga" Heleni na Jesika walishituka sana washawishika kumjua zaidi huyo Esilomu
aliwaeleza yote na ahadi ya yeye kukutana tena kesho aendelee kusimulia historia yake na kwa nini aliua, Jesika akasema "baba naomba na mimi kesho twende wote nikamuone je ukotayari"
mzee akafikiri kisha akatoa jibu kuwa kesho wataenda wote wawili.
ENDELEA...
Siku ya tatu toka hukumu itolewe yaani tarehe 23 mwezi wa aprili asubuhi siku hii palikuwa pametulia kabisa wana dar wakiwa katika mahangaiko yao wakijitaftia riziki, kila mmoja alionekana mtu mwenye matarajio ya kwenda mahari na kufanya kazi,
asubuhi hii nimoja kati ya asubuhi zinazo muogopesha sana Esilomu Ngwale ambae kulingana na hukumu inasema tarehe 25 mwezi aprili mwaka 2014 atanyongwa kwa kosa la kumuua makamu wa raisi na kumuua waziri wa mambo ya ndani alijiuliza sana akiwaza kulingana na habari kutoka kwa jaji Edisoni kuwa yuko tayari kumusaidia.
asubuhi ya saa mbili na nusu kutokana na saa iliyoko ukutani pale nyumbani kwa jaji
wakati huu jaji alikwisha jiandaa ili aweze kuelekea moja kwa moja huko jera kwenda kumalizia historia ya Esilomu
jaji akauliza " Jesika...? Jessi mama!!!"
"bee baba!!".
"ulisha maliza kujianda". baba aliuliza.
"ndiyo nilishamaliza" Jesika alijibu huku akiwa anafungua mlango wa chumba chake..
leo binti huyu alivalia mavazi mazuri ya hadhi ya juu sana nibinti mwenye mvuto wa hari ya juu kabisa kiasi kwamba ukimuona utadhani ni moja kati ya mis tanzania.
walimuaga mama yaani bi Heleni nakuondoka wakiwa njiani walianza kubadilishana mawazo " sasa baba kunakitu nilijiuliza jana usiku" jessi alisema.
"kuhusu nini? kuhusu hii kesi au nini?!" baba aliuliza
"ndiyo kuhusu hii kesi" jesika alikubari
"ulijiuliza nini?". baba aliuliza
"nilijiuliza kwamba hapa wanao jua ukweri wa mambo kumuhusu Essi ni sisi tuu na siku zinaisha reo tarehe 23 kesho 24 kesho kutwa 25 na hii tarehe 25 atanyongwa saa sita mchana baba wewe utafanya nini kumsaidia?" jesika aliuliza swari ambalo likawa gumu kwa jaji Eddi alinyamanza kidogo nakusema "mwanangu sijui nitafanya nini lakini najua lazima nitumie kila mbinu ili niweke mambo sawa, hukumu anatoa mimi ilapia ninamamulaka japo siyo ya kufuta kesi ila ninamamulaka nitayatumia halafu nione nikishindwa kunanjia moja tuu nitakayo fanya". Eddi alisema
Jessi pia akasema "aya baba mimi sina neno la kuongea zaidi"
waliendelea na safari huku wakiwa wanabadilishana mawazo.
Ni saa nne na dakika kumi na mbili kwa mjibu wa saa iliyo ndani ya gari yao saa hii walifika magareza,
moja kwa moja wakaenda kuonana na bwana jera
ndugu Shabani Rashid.
"karibu sana jaji" bwana jera alisema
"asante sana ndugu yangu" Eddi alisema
"vipi na huyu nani?" Shabani aluuliza akimunyoshea kidore Jesika
"Anaitwa jesika ni mwanangu alikuwa urusi kimasomo sasa karudi jana, Jesika huyu ni bwana jera wa hapa".
"nafurahi kumjua shikamo mzee?" jesika alisema.
"marahaba mwanangu tupo sana tupo mpaka nyumbani kwangu!!"bwana jera alisema huku akimuangalia Edisoni.
"Tutafika usijari kwa hata kule kwako ni nyumbani kwetu" jaji alisema .
muda kidogo kupita jaji akaongezea " vipi yule kijana naweza kumpata"
"yaa yupo mnaweza kwenda kumuona yuko kule kule ulipo muona jana!" bwana jera aliwaambia.
"tunashukuru sisi ngoja tufikepo". eddi alisema.
Baada ya dakika chache walifika alipo kuwa Esilomu Ngwale, muda huu alikuwa amejilaza mara akasikia sauti ya mulinzi akiwafungulia mlango Eddi na mwanae Jessi
Edison alishangaa sana kuona uzuri wa Jesika alio kuwa nao alishindwa kujizuia alianza kuuliza " huyu na..." hakumaliza jaji akasema ni mwanangu alikuwa huko urusi kimasomo kaja jana".
"ahaaaa sawa vizuri sana, binti habari?" Eddi alisema
"poa, pole na matatizo yaliyo kukuta mpaka uko hapa, jana baba aliniambia yote yaliyo kusibu nikashawishika nifike ili nami kwa kushirikiana na mzee tuone jinsi gani ya kukusaidia". Jesika alisema kwa kumkatisha mengi ambayo Eddi alitaka kuongea na kwa sababu ya jinsi alivyo kuwa akimuangalia.
"tusipoteze muda naomba basi utuelezee je, huyu jama kwa jina la Ishimael Shemley ambae alikuwa ni waziri wa mambo ya ndani,
naomba uniambie kwa nini nae ulimuua tafadhari endelea kusimulia".
"jaji nakuomba hata nikinyongwa hizi zote siri uziseme kwamba kwa nini niliua tafadhari nakuomba useme najua kuna uwezekano wa mimi kufa hata nikifa basi usisite kusema ukweri, ila usije ukasema kuwa sijaua wewe sema ila tuu nakuomba sema na sababu zilizo sababisha mimi kuua". eddi alisema huku macho yakianza kutokwa na machozi.
"usijari nitakusaidia eddi sawa?" jaji alisema.
huku akiwa analia eddi akaendelea na historia.
" Ishimael Shemley ni mtu alie kuwa akiishi Arusha kabla hajaja Dar es salaamu alikuwa mfanya biashara mkubwa sana kule Arusha alimiliki Hotel nyingi sana na alikuwa na Shule za sekondari biashara aliyo kuwa akiifanya ni kuuza wanawake na kuuza viungo vya wanawake matiti, na vitu mbalimbali kutoka katika mwili wa mwanamke huyu Ishimael Shemley alikuza wigo wa kazi akawa anauza wanawake njje ya nchi hii, kila Hoteli aliyo kuwa akimiliki pembeni yake palikuwa na sehemu wanawake walio kuwa wanajiuza, wengi wanawake na wasichana wamekufa kwa sababu ya kuumwa magonjwa ya zina kama ukimwi na mengineyo mengi, wanawake alikuwa anawapata vijijini kwa kisingizio kwamba anawachukua wasichana na kuwaajiri kwenye hoteli zake lakini baada ya kuwatoa vijijini wengine wanakufa na wengine wana potea na wengine kutoloka na kurudi nyumbani kwao wakiwa na mimba na wengi wakiwa na magonjwa kama vile ukimwi na mengineyo.
baada ya muda kadha huyu mtu alichaguliwa kuwa kiongozi na baada yakuchaguliwa alichaguliwa kuwa mbunge wa Arusha mjini na mwishoe akapewa uwaziri wa mambo ya ndani,
wengi tulidhani biashara ile angeiacha ila kumbe sawa na kuchukua moto na kuweka gesi ya kupikia.
aliendelea na biashara ya kuuza akina dada na kudhamini makundi mbalimbali ya ujambazi na wizi."
jaji alihisi kulegea baada ya kusikia hayo "heeeee kumbe pole sana, sasa kwanini ulimuua au nikwa sababu ya kuwa alikuwa anauza wanawake?" jaji aliuliza.
"Hapana nilimuua kwa sababu yeye kwa mjibu wa baba yangu anasema mama yangu ni moja kati ya watu walio kuwa wakiuzwa na Ishimael Shemley sasa baada ya kumuua mama yangu na huku baba hakuwa na uwezo wa kulipiza ndiyo sababu ya kwangu kumuua".
"du!! pole sana, je mama yako aliitwa nani?" Jesika ambae wakati wote alikuwa kimya aliuliza.
"baba alinionesha vitambulisho kuwa mama yangu si mtu wa kule Arusha bari ni mtu kutoka Kigoma alitoka kule kigoma kwa kudanganywa kuwa ameenda kule mjini kufanya kazi kwenye hoteli moja kule mjini ila baada ya kupelekwa mjini alicho ambulia ni kuuzwa na jina lake aliita Penina mtoto wa Mwasera"
jaji alistuka sana baada ya kusikia jina la Penina Mwasera.
"Penina Mwasera?"jaji aliuliza
"Ndiyo mwasera ni mtu kutoka kule kigoma aliishi kule lakini nilijalibu kwenda kule kigoma kufatilia ndugu na jama wa Mwasera sikumpata wala hata kupata mwelekeo nikabaki natapatapa nilikata tama" Eddison alisema.
kijasho kilimtoka Eddi hakuamini baada ya kulisikia jina la Penina Mwasera.
"umesema kuwa ni Penina Mwasera?". jaji aliuliza.
"ndiyo, kwani unamfahamu?"
eddi aliuliza.
"Ndiyo namjua tena namjua".
Edisoni alisema akiwa anatetemeka na machozi yakimtoka.
"namjua....namjua.... namjua
Penina Mwasera namjua kabisa namjua kabisa namjua"
jaji aliendelea kusema kwa pupa huku machozi yakichuruzika na akiwa anaria
kitendo ambacho kilimusisimua kila mmoja pale nakushangaa na kupata shauku la kujua nini kinaendelea na kumjua huyo Penina Ngware.
ITAENDELEA.........
MPENZI MSOMAJI TUKUTANE SEHEMU IJAYO INAYO ITWA HUKUMU YA HAKI.
LIKE AU COMMENT CHOCHOTE ILI NIJUE KAMA TUKO PAMOJA
.
BONYEZA HAPA