KIDNEY SIMULIZI......................KIDNEY MTUNZI.........Ayubu HD MAWASILIANO......+255746207667 Email:..Ayubuhenry25@gmail.com
☆
☆
☆
☆
☆
Mnamo saa mbili usiku binti Veronica Jumbe alikuwa akilisogelea gari lililokuwa mbele ya nyumba moja iliyokuwa na mwanga hafifu huku akitembea kwa kunyata ili asionekane, kutokana na mwanga hafifu wa eneo hili la kificho hakuonekana na mtu yeyote. Alizidi kulinyatia gari hili na akiwa anaangaza kila pande ili kama kuna mtu yeyote ambae anamuona "Nimejitolea kwa chochote ili mradi niwe na wewe najua umeteseka sana kunipata ila huwezi amini hata mimi nimeteseka sana kukupata, sijui nikuambie jambo gani ili unielewe ila naona sawa na kipofu aliekuwa jagwani na amepata bahati ya kupata mwokozi hakika ninafuraha kubwa moyoni kuwa na wewe, wakati mwingine natamani ningekuwa mafuta unayo jipaka ili wakati wote nikutie harufu nzuri ili wenye wivu wakome." sauti ya mwanaume ilisikika ndani ya gari huku Veronica akizidi kulisogelea na kua makini na kusikiliza kilicho kuwa kinaongelewa na watu waliokuwemo ndani ya gari hilo la kifahari. "Kenedi huu ni usiku na kama unakumbuka nyumbani sikuaga naomba unirudishe kwanza tutaongea kesho mchana nakuomba sana, baba atanitafta atakapo toka gengeni kila akija lazima anitafte na ukizingatia mimi nategemewa pale nyumbani, naomba sana" sauti ya kike ilisika ndani ya gari hili, Veronica baada ya kulisogelea gari hilo kabla hajajua ni nani nani wamo ndani ya gari, gari liliwashwa na kuondoka. bila kupoteza mda Veronica alikimbia kwa kasi na kuingia ndani ya gari alilokuwa amelisimamisha pembeni kidogo ya kinjia, aliwasha gali na kuikimbiza kwa kasi kulifuata gali lile alilokuwa na wasiwasi. kwa mwendo aliokuwa nao ilimchukua dakika chache kulifikia gali lile, moyo ulikuwa unamuenda kasi na kupata shauku la kujua kunanini kinaendelea, bila kupoteza hata dakika alikuwa nalo sambamba huku akichungulia ndani kutaka kujua kuna nani, kutokana na vio vya milango kufungwa ilikuwa ngumu kufanya utafiti huu au kugundua chochote kutokana na vio kuwa vya rangi nyeusi. kadiri dakika zilivyo zidikusonga mbele Veronika alikuwa anahisi kizungu zungu "Eeee Mungu naomba hari isijirudie tena" Veronika alikuwa akijiongelesha huku akimuomba Mungu. Mda wa dakika chache Veronica alishindwa kulifatilia kutokana na kuzidiwa na hari iliyo mkuta. alichukua simu na kumpigia rafiki yake kipenzi Maua "helloo veronica" sauti ilisikika "Maua hari imerudia tena na hapa natapatapa nahisi kizungu zungu sana naomba unifate sitaweza kufika nyumbani tafadhari naomba unisaidie" Veronica alisema "Pole Vero kwani uko wapi? jamani?" Maua aliuliza "njiani natokea njia ya huku mjini naomba unifate tafadhari" alisema na kukata simu "hello!? hello!?" Alibaki akiita lakini Veronica alikuwa kakata simu.
★
★
★
kwenye nyumba ya kifahari iliyo pambika kwa bustani za kupendeza na maua yanayo tia harufu ya marashi, "Vero? Vero amka basi" Sauti ya Maua kumuasha Veronica ilisikika dakika chache Vero aliamka "Kuna nini?"Vero aliuliza "mmh vipi vero umechanganikiwa au"Maua aliuliza "Kenedi yuko wapi?" Veronica aliuliza "wee vipi unaongea nini mbona sikuelewi? Kenedi yuko nyumbani kwake"Maua alijibu "Hapana hayupo nimemshuhudia yuko na mwanamke mwingine,!" Veronika alisema "Embu pumzika naona una kichaa wewe, Kenedi yuko nyumbani jamani". Maua alidai "Nakuambia hivi sina kichaa niko sawa ila nimemshudia kabisa." Veronika alisema "aya umemshuhudia wapi? na akiwa na nani?" Maua aliuliza "Nilikuwa nimetoka kwa dr Andason kwa bahati nikaona gari la Kenedi imesimamishwa pembeni kidogo ya nyumba ila karibu pia na njia, nikaamua kusimamisha gari langu na kuisogelea gari lile nikawasikia wakiongea ila sikubahatika kulifikia sababu nilipo karibia gari liliwashwa na kuondoka, sasa sijui kwa nini Kenedi kaamua kuniumiza kiasi hiki." Veronica alidai "Hapana vero usiwaze sababu kwanza huna uhakika wa jambo hili na katika maisha kuchukua uamzi wowote bila kuwa na uhakika ni makosa" Maua alisema "Maua siwezi kuelewa kabisa sababu kama..... jamani kwanini lakini afanye hivi wakati" Veronika alikosa pumzi akashindwa kuongea "Vero mbona unajitabisha kiasi hicho kwa kitu usichokua na uhakika wa jambo? embu angalia hari yako na ujaribu kupima ni kiasi gani unavyo jitaabisha embu jizuie jamani". Maua alisema huku akimshika mkono rafiki yake Veronika "Maua unajua mapenzi yanaumiza mbali na jinsi navyo umwa ila hawezi akanikosea kiasi hiki, anafahamu fika kuwa nampenda asinge nifanyia hivi jamani, Maua?" Veronica aliita "bee!!!" Maua aliitikia "Naomba nikalale kwanza sijisikii vizuri!" Veronika alisema "sawa, vipi hautakula sababu chakula tayari!?" Maua aliuliza "Usijari Maua asante lakini, hapa sijisikii kula chochote naomba nikalale tu!" Veronika alisema huku akisimama na kutembea kuelekea chumba chake kulala. Usiku mzima hakupata usingizi na alikuwa analia huku akiiangalia picha ya Kenedi iliyokuwa kwenye meza ndogo iliyokuwemo chumbani mwake. "Kenedi nakupenda na ndio sababu nikajitolea kufa kwa ajiri yako na sikutamani hata kidogo uumie wala ukwazike kisa mwili wangu wala maisha yangu, nilikukabidhi kila kitu ili mradi uwe na mimi na usiniache, sijui na siamini nilichosikia nahisi ni ndoto" Veronica alikua akiwaza huku anatoa sauti ya maneno. ★ ★ ★ ★ Saa tano na dakika kumi na moja kwa mjibu wa saa ya mkononi mwa Kenedi, "Haloo ?!" Kenedi aliitikia baada ya kupokea simu. "samahani Kenedi vipi unaweza kunisaidia mpenzi wangu? ila samahani!!" sauti ya upande wa pili ilisikika "Seda jamani embu kuwa huru mimi ni wako na kwa tatizo lolote niko radhi kukusaidia" Kenedi alisema "Asante sana Kenedi ila nisaidie kweri utaweza?" Seda binti anae pendwa na Kenedi alisema "sema jamani usiogope" Kenedi alisema "Kenedi naogopa kufa, namuogopa Veronica naomba umwache ili uishi na mimi tu. pia nisaidie milioni mbili tafadhari" Seda alisema "Seda, kwanza nikutoe wasiwasi Veronica mimi nimesha mwacha ila hajui tu acha pia hata hii pesa atoe yeye ili nikupe wewe. huwa namuangalia nashindwa kumuelewa mwili mwembamba kama kama kuni za masikini au mwiko wa kusongea ugari harafu eti awe na mimi si ujinga huo acha bwana hanijui, unajua hanijui mimi naitwa Kenedi mtoto nilie kulia shida hivyo hawezi nitisha" Kenedi alisema na kumfanya Seda afrahi na kushinda kujizuia akasema "siyo kila mwanamke wa tanga anajua mapenzi wengine ni uchafu kwa waume zao kila siku lawama zisizo isha". Seda alisema na kuzua uchambuzi wa kumchambua Veronica. Walimchambua Veronica na mwisho Seda alikata simu na Kenedi akaendelea na kazi zake nyumbani kwake. Dakika tano kupita simu iliita "Huyu anataka kuniambia nini?"Kenedi alijisemea moyoni huku anataka kupokea simu ile,***********
*
*
*
*
Usikose ijayo, fuatilia kisa hiki cha kusisimua like na comment ili tuwe pamoja. kidney ni simulizi iliyo beba ukweri wa baadhi ya watu, ni kisa ambacho sijui wewe unge fanya nini ukiwa mshiriki wa hayo au kama mapenzi yamesha kuumiza ulifanya ninu? fuatilia ujue kilicho tokea kwa wenzetu, Kenedi,Veronica,Seda na wengine wengi tu.